Skip to main content

Fahamu vitu 7 usivyo vijua kuhusu Ebola -Tanzania

1. EBOLA NI NINI?
Ebola ni ugonjwa wa hatari unaosababishwa na virusi vijulikanavyo kitaalam (Ebola Virus). Ugonjwa huu ni miongoni mwa magonjwa yajulikanayo kwa ujumla kama Homa za virusi zinazosababisha kutoka damu mwilini.
"Ugonjwa huu unaathiri binadamu na wanyama kama vile nyani, ngedere, sokwe na popo."

2. MTU ANAWEZAJE KUAMBUKIZWA VIRUSI VYA EBOLA?
Mtu anaweza kuambukizwa ugonjwa wa Ebola toka kwa mtu mwingine aliyeambukizwa, au toka kwa wanyama kama nyani, ngedere, sokwe na popo.
Ugonjwa wa Ebola unaambukizwa kwa haraka kutoka mtu mmoja hadi mwingine kupitia njia zifuatazo:-
• Kugusa majimaji ya mwili toka kwa mtu aliyeambukizwa virusi vya Ebola - damu, matapishi, jasho, mkojo, mate, machozi, kamasi
• Kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyefariki kwa ugonjwa wa Ebola
• Kugusa godoro, shuka, blanketi, au nguo zilizotumiwa na mgonjwa wa Ebola
• Kuchomwa na sindano au vifaa visivyo safi na salama
• Kugusa mizoga au kula wanyama pori kama vile Sokwe,nyani na popo
• Kula matunda yaliyoliwa nusu na Wanyama
 
3. Nani wapo katika hatari zaidi ya kupata ugonjwa wa Ebola?
Kila mtu yupo katika hatari ya kuambukizwa  na virusi vya Ebola, hata hivyo makundi ya watu wafuatao wapo kwenye hatari zaidi ya kuambukizwa virusi vya Ebola:
•  Watu wote wanaoishi na/ au kumhudumia mgonjwa wa Ebola
•  Waombolezaji ambao wanaweza kugusa mwili wa marehemu kama sehemu ya utaratibu wa mazishi
• Wawindaji wa msituni ambao wanaweza kugusa mizoga ya wanyama
• Watoa huduma za afya
 
4. Dalili za ugonjwa wa Ebola ni  zipi?
Dalili za ugonjwa wa Ebola huanza kujitokeza  kati ya siku 2 hadi 21 baada ya kupata  maambukizi. Mgonjwa wa Ebola huwa na  dalili zifuatazo:
      Homa kali ya ghafla
      Maumivu ya kichwa
      Maumivu ya mwili, misuli na viungo
      Kuharisha (kunakoweza kuambatana na
      damu)
      Kutapika (kunakoweza kuambatana na
      damu)
      Vipele mwilini
      Kutokwa na damu puani, mdomoni,
      machoni, masikioni na sehemu ya haja
      ndogo na kubwa
      Kuvia damu chini ya ngozi
 
5. Wakati gani mtu akapate  matibabu?
Nenda haraka kwenye kituo cha kutolea  huduma za afya pindi unapohisi kuwa na dalili  za ugonjwa wa Ebola, au unapogusana na mtu  mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola. Na pia, ni muhimu kutoa taarifa haraka kwenye kituo cha kutolea huduma za afya kilicho karibu nawe  pindi unapohisi mtu ana dalili za ugonjwa wa Ebola.
 
6. Je, ugonjwa wa Ebola unatibika?
Ugonjwa wa Ebola hauna tiba maalum wala chanjo. Mgonjwa anashauriwa kuwahi  kituo cha kutolea huduma ya afya ili aweze kupatiwa tiba saidizi kulingana na dalili alizonazo kama vile:
      Tiba ya homa na maumivu
      Kuongezewa maji mwilini
      Tiba lishe 
7. Nifanye nini ili kujikinga na ugonjwa wa Ebola?
Njia za kujikinga na ugonjwa huu ni :-
      Epuka kusalimiana kwa kushikana mikono au kukumbatiana
      Epuka kugusa damu, matapishi, mkojo, kinyesi, kamasi, mate, machozi na maji maji mengine yanayotoka mwilini mwa mtu mwenye dalili za ugonjwa huu
      Epuka kugusa au kuosha maiti ya mtu aliyekufa akiwa na dalili za Ebola badala yake toa taarifa kwa uongozi wa serikali ili wasimamie taratibu za mazishi
      Epuka kutumia nguo, shuka, blanketi, kitanda na godoro za mtu aliyeambukizwa ugonjwa huu
Nawa mikono kwa maji yanayotiririka na sabuni mara unapomtembelea mgonjwa hospitalini au kumhudumia nyumbani
      Epuka kugusa wanyama kama vile popo, nyani, sokwe, tumbili na swala au mizoga ya wanyama
      Zingatia ushauri na maelekezo yanayotolewa na wataalamu wa afya na viongozi wa serikali kuhusu ugonjwa wa Ebola
      Wahi kituo cha kutolea huduma za afya uonapo dalili za ugonjwa wa Ebola
      Toa taarifa mapema kwenye kituo cha huduma za afya, ofsi ya serikali ya mtaa au kijiji uonapo mtu mwenye dalili za ugonjwa wa Ebola au kifo.
      Zingatia usafi binafsi pamoja na usafi wa mazingira yako.


-manyanda health

Comments

Popular posts from this blog

FAHAMU KILA KITU KUHUSU MAGONJWA YA MOYO

LEO tutaelezea kwa kina chanzo cha magonjwa ya moyo ambayo husumbua watu wengi. Chanzo kikubwa ni watu kutozingatia kanuni za ulaji bora, ni moja ya mambo yanayoongeza uwezekano wa mtu kupata magonjwa ya moyo. Kwa mfano, ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, vyakula vyenye sukari nyingi, chumvi nyingi na lehemu nyingi , huku ulaji wa mbogamboga na matunda ukiwa ni wa kiwango cha chini, huongeza uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo. Lakini pia hali ya kuwa na uzito uliozidi kiasi au kuwa na unene uliopitiliza pamoja na kutofanya mazoezi ya mwili na viungo mara kwa mara, huchochea uwezekano wa mtu kukumbwa na magonjwa ya moyo. Wakati mwingine magonjwa ya moyo huweza kutokana na historia ya ugonjwa huo katika familia. Umri unapozidi miaka 50 kuna uwezekano pia wa kupatwa na magonjwa haya ya moyo, huku wanaume wakiwa kwenye hatari zaidi ya kupatwa na tatizo hili mapema zaidi ikilinganishwa na wanawake. Magonjwa ya moyo huanza kumwandama mtu pale mambo fulani ...

ULAJI WA VYAKULA HIVI UNAWEZA KUPELEKEA UTASA KWA ZAIDI YA 18%

MAKALA FUPI | BROZ MEDIA TZ Mwanamke ambaye ana mazoea ya kula vyakula vyenye mafuta mengi na sukari bila ya kutumia matunda kwa wingi, yumo kwenye hatari ya kutopata uja uzito, utafiti unasema . Utafiti uliofanyiwa wanawake 5,598, uliwapata wale ambao wana mazoea ya kula vyakula vyenye mafuta mengi, mara 4 au zaidi kwa wiki, wanachukua zaidi ya mwezi mmoja kupata uja uzito, kuliko wanawake ambao hawatumii kabisa chakula cha aina hiyo. Walaji wengi wa chakula cha aina hiyo, pia sio rahisi kupata mimba, katika kipindi cha mwaka mzima, hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya uzazi wa binadamu. Wataalamu wanasema kwamba, lishe bora huboresha uwezekano wa kushika mimba. Hata hivyo, kumekuwa na changamoto fulani na utafiti huo, ukiwemo swala la wanawake kujaribu kukumbuka, kile walichokuwa wa kila wakati wana uja uzito. Wanawake nchini Australia, New Zealand, Ireland na Uingereza, waliulizwa kuhusiana na kile walichokuwa wakila mwezi mmoja kabla ya kushika mimba, hasa...

Fahamu vyakula vinavyo weza sababisha mwanamke kuwahi kufikia ukomo wa hedhi

  Utafiti umebaini ulaji wa tambi na wali kwa wingi husababisha ukomo wa hedhi mapema Vyakula vyenye wanga kwa wingi husababisha wanawake kukoma hedhi mapema , utafiti umeeleza. Ulaji wa tambi na wali kwa wingi kwa wanawake nchini Uingereza kunasababisha kuwahi kukoma kwa hedhi mwaka mmoja na nusu mapema zaidi ya wastani wa umri wa miaka 51 . Hata hivyo, utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Leeds kwa wanawake 914 nchini Uingereza , pia umebaini kuwa mlo ulio na mafuta ya samaki kwa wingi na njegere na maharage unaweza kuchelewesha ukomo wa hedhi kwa wanawake. Lakini wachambuzi wanasema kuna sababu nyingine, zikiwemo jenetiki Haijafahamika ni kwa ukubwa gani ulaji chakula unaweza kuleta athari kwa wanawake kama tafiti zinavyoeleza. Utafiti ulichapishwa kwenye jarida la Afya la Epidemiology & Community Health na wanawake waliulizwa mlo wao huwa una vyakula gani Mlo wenye mboga za jamii ya kunde kwa wingi, kama vile njegere,maharage,maharage membamba na...