Skip to main content

ULAJI WA VYAKULA HIVI UNAWEZA KUPELEKEA UTASA KWA ZAIDI YA 18%

MAKALA FUPI |BROZ MEDIA TZ
Mwanamke ambaye ana mazoea ya kula vyakula vyenye mafuta mengi na sukari bila ya kutumia matunda kwa wingi, yumo kwenye hatari ya kutopata uja uzito, utafiti unasema.

Utafiti uliofanyiwa wanawake 5,598, uliwapata wale ambao wana mazoea ya kula vyakula vyenye mafuta mengi, mara 4 au zaidi kwa wiki, wanachukua zaidi ya mwezi mmoja kupata uja uzito, kuliko wanawake ambao hawatumii kabisa chakula cha aina hiyo.
Walaji wengi wa chakula cha aina hiyo, pia sio rahisi kupata mimba, katika kipindi cha mwaka mzima, hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya uzazi wa binadamu.
Wataalamu wanasema kwamba, lishe bora huboresha uwezekano wa kushika mimba.

Hata hivyo, kumekuwa na changamoto fulani na utafiti huo, ukiwemo swala la wanawake kujaribu kukumbuka, kile walichokuwa wa kila wakati wana uja uzito.
Wanawake nchini Australia, New Zealand, Ireland na Uingereza, waliulizwa kuhusiana na kile walichokuwa wakila mwezi mmoja kabla ya kushika mimba, hasa wakati wa mimba yao ya kwanza.
Wakunga waliwatembelea kina mama hao, walipokuwa na mimba ya wiki 14 hadi 16, na wakaulizwa ni mara ngapi walikula matunda, mboga za majani na samaki, mbali na chakula kama burgers, pizza, kuku wa kukaangwa pamoja na vibanzi, kutoka katika migahawa inayouza vyakula vya mafuta mengi na sukari.
Watafiti hao walibaini kuwa, wanawake wanaotumia matunda mara tatu kwa mwezi, wanachukua kiwango cha nusu mwezi kwa wastani kushika mimba, kuliko wale ambao wamekula matunda mara tatu au zaidi kwa siku.

Pia walipiga hesabu kuwa, ''wanawake walio na kiwango kidogo mno cha ulaji wa matunda mwilini, wako kwenye hatari ya 12% ya kutokuwa na uwezo wa kushika mimba katika kipindi cha chini ya mwaka mmoja, huku hali kama hiyo ni asilimia 16% ya wale ambao wamekula chakula kilicho na mafuta mengi, mara nne au zaidi kwa wiki.
Hii kwa ujumla ni hatari kwa asilimia 8% katika kundi sawa na hilo.''
Watu waliooana hawakutumika katika utafiti huu, hasa ikiwa mpenzi wa kiume alikuwa akipokea matibabu ya uzazi.
Mhadhiri Claire Roberts, kutoka Chuo kikuu cha Adelaide, Australia, ambaye aliongoza jopo la watafiti hao, anasema: "Matokeo hayo, yanaonyesha kuwa, ulaji chakula bora, kinachojumuisha matunda na upungazaji wa chakula chenye mafuta mengi na sukari, yatapunguza pakubwa muda wa kushika mimba kwa wanawake."

Hata hivyo, huku watafiti hao wakipata uhusiano uliopo kati ya utumiaji wa matunda na chakula chenye mafuta mengi, kwa uwiano wa muda unaochukua mwanamke kutunga mimba, lakini cha ajabu utafiti wao haukupata chochote dhidi ya uhusiano wa ulaji maboga na samaki.
Daktari Gino Pecoraro, mhadhiri mkuu wa Chuo Kikuu cha Queensland, ambaye hakujumuishwa katika utafiti huo, anasema kuwa, "Kwa ujumla, utafiti huo, hauungi mkono, jinsi wataalamu wa vyakula, wanavyoamini - wanaosema kuwa vyakula vyenye lishe bora, ni vizuri kwa wanandoa kuwasaidia kupata mimba."


-bbc swahili

Comments

Popular posts from this blog

FAHAMU KILA KITU KUHUSU MAGONJWA YA MOYO

LEO tutaelezea kwa kina chanzo cha magonjwa ya moyo ambayo husumbua watu wengi. Chanzo kikubwa ni watu kutozingatia kanuni za ulaji bora, ni moja ya mambo yanayoongeza uwezekano wa mtu kupata magonjwa ya moyo. Kwa mfano, ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, vyakula vyenye sukari nyingi, chumvi nyingi na lehemu nyingi , huku ulaji wa mbogamboga na matunda ukiwa ni wa kiwango cha chini, huongeza uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo. Lakini pia hali ya kuwa na uzito uliozidi kiasi au kuwa na unene uliopitiliza pamoja na kutofanya mazoezi ya mwili na viungo mara kwa mara, huchochea uwezekano wa mtu kukumbwa na magonjwa ya moyo. Wakati mwingine magonjwa ya moyo huweza kutokana na historia ya ugonjwa huo katika familia. Umri unapozidi miaka 50 kuna uwezekano pia wa kupatwa na magonjwa haya ya moyo, huku wanaume wakiwa kwenye hatari zaidi ya kupatwa na tatizo hili mapema zaidi ikilinganishwa na wanawake. Magonjwa ya moyo huanza kumwandama mtu pale mambo fulani ...

Fahamu vyakula vinavyo weza sababisha mwanamke kuwahi kufikia ukomo wa hedhi

  Utafiti umebaini ulaji wa tambi na wali kwa wingi husababisha ukomo wa hedhi mapema Vyakula vyenye wanga kwa wingi husababisha wanawake kukoma hedhi mapema , utafiti umeeleza. Ulaji wa tambi na wali kwa wingi kwa wanawake nchini Uingereza kunasababisha kuwahi kukoma kwa hedhi mwaka mmoja na nusu mapema zaidi ya wastani wa umri wa miaka 51 . Hata hivyo, utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Leeds kwa wanawake 914 nchini Uingereza , pia umebaini kuwa mlo ulio na mafuta ya samaki kwa wingi na njegere na maharage unaweza kuchelewesha ukomo wa hedhi kwa wanawake. Lakini wachambuzi wanasema kuna sababu nyingine, zikiwemo jenetiki Haijafahamika ni kwa ukubwa gani ulaji chakula unaweza kuleta athari kwa wanawake kama tafiti zinavyoeleza. Utafiti ulichapishwa kwenye jarida la Afya la Epidemiology & Community Health na wanawake waliulizwa mlo wao huwa una vyakula gani Mlo wenye mboga za jamii ya kunde kwa wingi, kama vile njegere,maharage,maharage membamba na...