Skip to main content

Fahamu vyakula vinavyo weza sababisha mwanamke kuwahi kufikia ukomo wa hedhi

 
Utafiti umebaini ulaji wa tambi na wali kwa wingi husababisha ukomo wa hedhi mapema
Vyakula vyenye wanga kwa wingi husababisha wanawake kukoma hedhi mapema, utafiti umeeleza.
Ulaji wa tambi na wali kwa wingi kwa wanawake nchini Uingereza kunasababisha kuwahi kukoma kwa hedhi mwaka mmoja na nusu mapema zaidi ya wastani wa umri wa miaka 51.
Hata hivyo, utafiti uliofanywa na Chuo kikuu cha Leeds kwa wanawake 914 nchini Uingereza , pia umebaini kuwa mlo ulio na mafuta ya samaki kwa wingi na njegere na maharage unaweza kuchelewesha ukomo wa hedhi kwa wanawake.

Lakini wachambuzi wanasema kuna sababu nyingine, zikiwemo jenetiki
Haijafahamika ni kwa ukubwa gani ulaji chakula unaweza kuleta athari kwa wanawake kama tafiti zinavyoeleza.
Utafiti ulichapishwa kwenye jarida la Afya la Epidemiology & Community Health na wanawake waliulizwa mlo wao huwa una vyakula gani
Mlo wenye mboga za jamii ya kunde kwa wingi, kama vile njegere,maharage,maharage membamba na dengu kwa wastani huchelewesha ukomo wa hedhi
Vyakula vya wanga,hasa wali na tambi, vimeelezwa kusababisha ukomo wa hedhi mapema zaidi. 

Sababu nyingine zilizoainishwa na watafiti ni pamoja na uzito wa mwanamke, Historia ya uzazi na waliopata tiba za homoni, lakini hawakuangalia sababu za kijenetiki
Janet Cade ni mtaalam wa lishe, anasema umri ambao ukomo wa hedhi huanza unaweza ''kuleta madhara makubwa'' kwa baadhi ya wanawake.

Wanawake ambao hedhi zao hukoma mapema wako kwenye hatari ya kupata maradhi ya moyo na maradhi ya mifupa, na wanaochelewa wanaweza kupata maradhi ya saratani ya matiti,tumbo na Ovari
Vyakula jamii ya kunde vinaelezwa kuchelewesha ukomo wa hedhi kwa wanawake
Wataalam wanasema kwa bahati mbaya tafiti hizi za kiuchunguzi zina changamoto ya kuthibitisha kama mlo husababisha ukomo wa hedhi mapema, mpaka pale ushahidi utakapoonekana, hivyo hakuna haja ya watu kubadili mlo. 

source: bbc

Comments

Popular posts from this blog

FAHAMU KILA KITU KUHUSU MAGONJWA YA MOYO

LEO tutaelezea kwa kina chanzo cha magonjwa ya moyo ambayo husumbua watu wengi. Chanzo kikubwa ni watu kutozingatia kanuni za ulaji bora, ni moja ya mambo yanayoongeza uwezekano wa mtu kupata magonjwa ya moyo. Kwa mfano, ulaji wa vyakula vyenye mafuta mengi, vyakula vyenye sukari nyingi, chumvi nyingi na lehemu nyingi , huku ulaji wa mbogamboga na matunda ukiwa ni wa kiwango cha chini, huongeza uwezekano wa kupatwa na magonjwa ya moyo. Lakini pia hali ya kuwa na uzito uliozidi kiasi au kuwa na unene uliopitiliza pamoja na kutofanya mazoezi ya mwili na viungo mara kwa mara, huchochea uwezekano wa mtu kukumbwa na magonjwa ya moyo. Wakati mwingine magonjwa ya moyo huweza kutokana na historia ya ugonjwa huo katika familia. Umri unapozidi miaka 50 kuna uwezekano pia wa kupatwa na magonjwa haya ya moyo, huku wanaume wakiwa kwenye hatari zaidi ya kupatwa na tatizo hili mapema zaidi ikilinganishwa na wanawake. Magonjwa ya moyo huanza kumwandama mtu pale mambo fulani ...

ULAJI WA VYAKULA HIVI UNAWEZA KUPELEKEA UTASA KWA ZAIDI YA 18%

MAKALA FUPI | BROZ MEDIA TZ Mwanamke ambaye ana mazoea ya kula vyakula vyenye mafuta mengi na sukari bila ya kutumia matunda kwa wingi, yumo kwenye hatari ya kutopata uja uzito, utafiti unasema . Utafiti uliofanyiwa wanawake 5,598, uliwapata wale ambao wana mazoea ya kula vyakula vyenye mafuta mengi, mara 4 au zaidi kwa wiki, wanachukua zaidi ya mwezi mmoja kupata uja uzito, kuliko wanawake ambao hawatumii kabisa chakula cha aina hiyo. Walaji wengi wa chakula cha aina hiyo, pia sio rahisi kupata mimba, katika kipindi cha mwaka mzima, hayo ni kwa mujibu wa ripoti ya uzazi wa binadamu. Wataalamu wanasema kwamba, lishe bora huboresha uwezekano wa kushika mimba. Hata hivyo, kumekuwa na changamoto fulani na utafiti huo, ukiwemo swala la wanawake kujaribu kukumbuka, kile walichokuwa wa kila wakati wana uja uzito. Wanawake nchini Australia, New Zealand, Ireland na Uingereza, waliulizwa kuhusiana na kile walichokuwa wakila mwezi mmoja kabla ya kushika mimba, hasa...